ROSE MUHANDO HR BANNER

ROSE MUHANDO HR BANNER

ROSE MUHANDO SONG OF THE WEEK

MAONO YANGU [MY VISION & MISSION]

Namshukuru Mungu kwa kuniweza kunipa maono haya ambayo natumaini yanaweza kumtukuza Mungu. Ninampango wa kuanzisha semina kwaajili ya vijana. Semina hizi zitakuwa kuwajenga vijana kiroho na kumjua Mungu. Nimeona makanisani vijana wanapungua kutokana na kukosa kupata watu waliokaribu nao na wanaweza kuwajenga kiimani. Kanisa ni kubwa sana na lina mambo mengi ya kulea kondoo kwahiyo mara nyingi vijana wamekuwa wakiachwa hawana muelekeo na baadae kukataa tamaa ya kuendelea na wokovu na kujiingiza makundi ambayo hayamtukuzi Mungu na mwisho wake kupatwa na majanga mbalimbali.


Nilipokaa chini nikaona hakuna sababu ya kuwapoteza hawa vijana na kuliacha kanisa linaanguka. Makanisani kumejaa sana wazee na wale waliovuka ujana, na hii inaashiria kuwa baada ya miaka kadhaa kanisa litaanguka kwani wazee watakuwa wamechoka kufanya kazi ya Mungu.

Vijana wamekuwa wanakimbia kwaya na kuanza kuimba nyimbo za kijamii, na hii inatoka na kukosa watu wa kuwatia moyo na kuonyesha utamu wa kumuimbia Mungu. Hakuna watu wanaoweza kuwahamasisha vijana kufanya kazi ya Mungu. ha hii imesambaaa sana vijijini, vijana wengi vijijini wamemuacha Yesu na kushiriki matendo yasiompendeza Mungu. Kwahiyo nimeona ni vizuri nianzishe semina ambazo zitawafanya vija wafurahie wokovu na wampende Yesu.

No comments:

Post a Comment

HABARI ZILIZOPITA

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...